The House of Favourite Newspapers

Mama Samia: Serikali Kuendeleza Miradi ya Maji ‘Kumtua Mama Ndoo Kichwani’ – Video

0
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.

LEO Machi 8, 2020 ni siku ya Kimataifa ya Wanawake siku ambayo dunia inathamini mchango wa Wanawake katika jamii huadhimishwa tarehe 8, Machi ya kila mwaka na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kizazi cha Usawa kwa Maendeleo ya Tanzania ya Sasa na Baadae”.

Maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Simiyu mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan. 

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameitaka Halmashauri ya Mji wa Bariadi kutumia mapato yatakayotokana na stendi mpya ambayo inatarajia kukusanya mililoni 300 kwa mwaka katika shughuli za maendeleo ya wananchi.

Katika hotuba yake Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameyasema haya;-

“Tuliwapa maelekezo Benki ya Posta kufungua dirisha maalum kwa ajili kuwahudumia wanawake kama ilivyokuwa benki ya wanawake na wanafanya vizuri, kati ya Agosti 2018-Machi 2019 zaidi ya Tsh Bil. 2 zimetolewa kwa wanawake wajasiriamali.

“Ili Mwanamke aweze kufanya shughuli zake za kiuchumi na kijamii, anahitaji Umeme, Mpango wa kusambaza umeme vijijini unampa mwanamke mwanga na nuru na kumfungua katika maendeleo yake, tutumie fursa hii iliyoletwa na Serikali kwa manufaa.

“Katika kuhakikisha tunampa nafuu mwanamke katika kufanya shughuli zake, Serikali inatekeleza miradi mikubwa na maji kote nchini lengo ni kumtua mama ndoo kichwani na kuondoa changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji.
“Hatuna budi kuwakumbuka wanawake wote waliotangulia mbele za haki kwa kazi kubwa walizozifanya, na tuwaombee wote walio vitandani wapate nafuu ili waendelee na shughuli zao.
“Wanawake tuhimizane kuwaunga mkono Wanawake wenzetu hatimaye twende kwa wingi kupiga kura kuwachagua viongozi wenye muelekeo wa kutuletea maendeleo.
“Kwa kipindi hiki tunapoelekea uchaguzi Mkuu, nawahimiza wanawake wenzangu kujitokeza kwa wingi kiujiandikisha kwenye daftari la kupiga kura, kuchukua fomu na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Leave A Reply