Mamia Wamzika Akilimali wa Yanga Tandale Dar (Picha +Video)
MAZIKO ya aliyekuwa Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga, Ibrahim Akilimali yamefanyika leo Desemba 15, katika Msikiti wake wa Baraqat uliopo Tandale jijini Dar es Salaam baada ya kufikwa na umauti Jana Jumamosi, Desemba 14, 2019 katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo.
Katika maziko hayo ya Mzee Akilimali yalihudhuriwa na mamia ya watu wakiwemo mashabiki, wachezaji, viongozi wa klabu za Simba na Yanga pamoja na viongozi wa kisiasa.
Yanga alikuwepo Mwenyekiti wa klabu hiyo, Dk Mshindo Msolla, Katibu Mkuu, Dk David Ruhago na Ofisa Mhamasishaji, Antonio Nugaz.
Wengine ni aliyekuwa Mratibu wa timu hiyo, Hafidh Saleh pamoja na wanachama mbalimbali. Kwa upande wa Simba alikuwepo mwenyekiti wa zamani wa timu hiyo, Hassan Dalali na aliyekuwa Mbunge wa zamani wa Kinondoni, Idd Azzan.