Na GABRIEL NG`OSHA| GAZETI LA AMANI| SHOWBIZ XTRA
MAKUBWA! Kufuatia ugumu wa maisha kwenye tasnia ya sanaa nchini, msanii wa filamu Bongo, Fatuma Ayubu Bozi, ’ ameibukia kwenye Muziki wa Singeli na yupo mbioni kuibuka na wimbo mpya.
Akizungumza na Showbiz Xtra, Bozi ambaye pia ni muuza nyago kwenye video za Kibongo alisema kuwa, alishauriwa kuimba na msanii wa Singeli, Man Fongo baada ya kuona soko la filamu linafanya vibaya kwa kipindi hiki.
“Filamu hazilipi kwa sasa kama zamani na hali ya maisha ni ngumu, ni bora niimbe Muziki wa Singeli kama alivyonishauri Man Fongo nitatoka tu,” alisema Bozi.
Comments are closed.