The House of Favourite Newspapers

Manji, Gwajima Waondolewa Sentro, Huenda Wamepelekwa kwa Mkemia Mkuu

Taarifa zinaeleza Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji na Askofu Josephat Gwajima wameondolewa katika kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam.
Mmoja wa mashuhuda amesema Manji na Gwajima wanaweza wakawa wamepelekwa kupimwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali au Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
 
“Ni kweli hii saa kumi na nusu au zaidi, wameondolewa hapa kituoni. Wawili wamepanda gari aina ya Land Cruiser wakiongozana na askari Polisi kadhaa.
 
 
“Gari limeondoka na kuekelea maeneo ya Posta ya zamani. Huu uelekeo huenda kwenye ofisini za mkemia mkuu. Lakini hakuna mwenye taarifa rasmi,” kilieleza chanzo.
Manji na Gwajima walifika kwa ajili ya kuhojiwa kuhusiana na suala la madawa ya kulevya baada ya kutuhumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Save

Save

Comments are closed.