Mbeya: Wakili Mwabukusi Na ‘Mdude’ Waachiwa Kwa Dhamana
Wakili Boniface Mwabukusi na Mwanachama wa CHADEMA Mpaluka Nyagali (Mdude) wameachiwa kwa dhamana baada ya kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mbeya kwa siku kadhaa tangu walipokamatwa Mkoani Morogoro
Philip Mwakilima ambaye ni Wakili wa Mwabukusi na Mdude, amesema Watuhumiwa hao wawili wamebadilishiwa mashtaka kutoka Uhaini kuwa Uchochezi na watatakiwa kuripoti tena Kituo cha Polisi August 21, 2023