Aidha, zoezi la uokoaji wa abiria waliokuwemo katika kivuko cha MV Nyerere kilichozama lilisitishwa jana usiku kutokana na giza na litaendelea tena leo ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela amesema mpaka sasa watu waliookolewa wakiwa hai ni 37 na waliopoteza maisha ni 44.
“Kuna kivuko kinachounganisha kati ya Kisiwa cha Ukara na Ukerewe, kina hudumia zaidi ya wananchi 50,000, kimekuwa kikileta shida mara kwa mara, nimekuwa nikiwasiliana na wizara mara kwa mara, hatupendi kuja kuomba rambirambi kwa sababu ya wananchi kuzama kwenye kivuko kile.
“Tangu mwaka jana tuliahidiwa kwamba mpaka Desemba mashine mbili ambazo zilikuwa zimeagizwa zingekuwa zimeshafungwa lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea. Niombe kauli ya serikali, ni lini mashine hizo zitafungwa ili kivuko hicho kitoe huduma katika mazingira ya usalama.
Comments are closed.