Mdalasini, Asali kwa Kutuliza Kikohozi na Homa
Leo tutaongelea kiungo cha mdalasini kinavyosaidia kutibu ugonjwa wa kukohoa na homa ambapo ni rahisi kutengeneza nyumbani kwako na kukutibu kabisa.
Jinsi ya kutengeneza kama dawa
Chukua mdalasini usage, pata unga wake kijiko kimoja, baada ya hapo chukua asali kijiko kimoja kikubwa changaya kwa pamoja.
Jinsi ya kutumia
Ukishapata mchanganyiko huo, kunywa asubuhi, mchana na jioni kijiko kimoja kikubwa.
Unaweza kutengeneza tiba hii kulingana na siku yaani ukachukua vijiko vitatu vya unga wa mdalasini na asali vitatu kwa ajili ya siku nzima kisha kesho yake ukatengeneza mchanganyiko mwingine.
Faida ya dawa hii
Hutuliza kikohozi kwa haraka sana, pia huondoa homa kwa mtu mwenye homa kali, lakini mbali na kutibu magonjwa haya kama tujuavyo, tiba hii ukichangaya na maji ya vuguvugu na kunywa kila siku asubuhi huwa ni tiba nzuri ya kukata tumbo.
Lakini pia husaidia kusawazisha sukari mwilini na kuwa kama inavyotakiwa.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz