The House of Favourite Newspapers

Mfungwa Aliyemshambulia R Kelly Adai Alitumwa na Serikali

0

HATIMAYE mfungwa aliyemshambulia mwimbaji wa RnB duniani, Robert Kelly. maarufu R Kelly wakiwa gererani amejitokeza na kuzungumza sababu hasa za kumshambulia mwimbaji huyo.

 

Mfungwa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Jeremiah Shane Farmer (39) amesema alitumwa na serikali kufanya shambulizi hilo la kumdhuru R Kelly,

 

“Serikali ilinifanya nimshambulie R. Kelly,” alisema Jeremiah.

 

Kwa mujibu wa The Blast, Jeremiah, ametambulika kuwa ni mmoja kati ya memba hatari wa kundi la kihalifu maarufu kama Latin Kings.

 

Sambamba na hilo, Jeremiah alidai kuwa alifanya tukio hilo kwa lengo la kupata umaarufu na dunia kufahamu kwamba serikali inanuka rushwa.

 

Leave A Reply