Mgahawa Dar wanusulika kuungua
Mlango wa jengo hilo.
Moshi ukiwa umetanda ndani ya chumba cha mgahawa huo.
Gari la jeshi la zimamoto likiwa eneo la tukio.
Baadhi ya wananchi waliofika eneo hilo wakishuhudia uokoaji.
Moja ya friji lililokuwemo ndani likitolewa.
Likiwa limeungua.
Kikosi cha zimamoto kikiwa kazini.
Mmiliki wa jengo hilo, Hussein Said akihojiwa na wanahabari juu ya chanzo cha moto huo
Baadhi ya viti na meza vilivyokuwemo ndani ya mgahawa huo.
MGAHAWA mmoja uliopo ndani ya jengo la ghorofa sita lililopo mtaa wa Lumumba mkabala na Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, umenusurika kuungua baada ya kutokea hitilafu ya umeme iliyodaiwa chanzo chake ni waya wa friji ulioshika cheche za moto na kuwaka.
Akizungumza na mwanahabari wa mtandao huu, mmiliki wa jengo hilo, Hussein Said alisema hitilafu hiyo ilianzia katika chumba cha mgahawa kilichopo chini na hakuna aliyejeruhiwa zaidi ya kuungua kwa baadhi ya viti na vyombo.
Alisema kikosi cha zimamoto kilifika eneo la tukio kwa muda muafaka na kuuzima moto huo usisambae wala kuleta athari nyingine yoyote
Na Denis Mtima/Gpl