The House of Favourite Newspapers

Michirizi Ya Damu – 03

0

Walichanganyikiwa, ilikuwaje muuaji wa Belleck awe yule msichana aliyefanya mauaji kule nchini Misri na wakati mtu huyo alikuwa akitafutwa kila kona nchini humo?

Alishangaa. Hakutaka kutulia, haraka sana akatafuta namba ya simu ya mkuu wa polisi nchini Misri kupitia kitengo cha Interpool na kumuuliza kuhusu suala lile kama muuaji alikamatwa au la.

“Bado hatukumkamata!”
“Basi sawa.”
“Kuna nini?”

“Amefanya mauaji na huku pia.”
“Amefanya mauaji! Lini?”
“Leo hii!”
“Haiwezekani! Hakuna mtu anayeweza kuua kirahisi, ndani ya siku chache kama hizi,” alisema polisi mkuu kutoka nchini Misri.

“Ndicho kilichotokea! Ila nahisi tutampata japokuwa swali moja muhimu la kujiuliza, hivi kwa nini anaua mabilionea tu?” aliuliza polisi wa Ufaransa.

“Mmh! Kweli! Napata picha! Kwa nini mabilionea? Hii inamaanisha ndani ya siku chache zijazo kutakuwa na bilionea mwingine atauawa kama tu tusipofanya kazi ya ziada kumkamata?”

“Inawezekana! Hebu tusubiri. Ila nina uhakika kwa mauaji aliyoyafanya hapa, tutamkamata! Tena wiki hiihii na atatuambia kwa nini anauacha ujumbe huu kila anapofanya mauaji,” alisema polisi wa Ufaransa na kukata simu. Msako wa kumtafuta mwanamke huyo ukaendelea.

****

“Where is the father?” (padri yupo wapi?) alisikika msichana mmoja akiuliza kanisani alipokwenda kwenye chumba kidogo kwa ajili ya kuzungumza na padri lakini bahati mbaya hakumkuta.

“He was right there,” (alikuwa huko)

“Where?” (wapi?)

Watu walikuwa wakiulizana kanisani. Hakukuwa na watu wengi, kanisa zima lilikuwa na washirika watano ambao walikaa kwa kujigawa ndani ya kanisa hilo kubwa.

Walishangaa, kitendo cha kutokumuona padri kanisani humo kiliwapa wakati mgumu wa kutokugundua mwanaume huyo alikuwa wapi kwani kwa siku kama hiyo, tena ya kuungama dhambi zao, ilikuwa ni lazima padri awepo ndani ya chumba kile cha kuungamia dhambi.

Hakukuwa na mtu aliyejua mahali alipokuwa ila hawakuwa na hofu hata kidogo kwani waliamini kwamba padri huyo angerudi kanisani hapo na mambo kuendelea kama kawaida.

Hilo lilikuwa kanisa kubwa jijini New York nchini Marekani. Watu wengi wa Kanisa la Roma walikuwa wakishiriki misa katika kanisa hilo kubwa, wengi walitoka nchini nyingine na kufika katika kanisa hilo ambalo lilikuwa la kwanza kutembelewa na Papa José Kentenich miaka ya 1880.

Siku ya kwanza ikapita lakini hakukuwa na mtu aliyefahamu mahali padri alipokuwa. Walikuwa wakishiriki misa lakini kanisa liliongozwa na padri msaidizi ambaye naye hakujua mahali padri mkuu alipokuwa.

Wakati siku ya tatu ikiwa imeingia ndipo kanisani kukaanza kusikika harufu mbaya. Ilikuwa ni harufu ya mzoga iliyokuwa ikiwasumbua, wengi walihisi kwamba inawezekana mzoga huo ulikuwa nje ya kanisa hilo lakini kila walipokaa, wakajua kabisa mzoga huo ulikuwa ndani ya kanisa hilo.

Hapo ndipo walipoanza kuchunguza, waliangalia huku na kule na mwisho wa siku kugundua kwamba mzoga huo ulikuwa ndani ya chumba kile cha kuungamia dhambi ambacho kiliruhusiwa kuingiwa na mtu mmoja tu ambaye ndiye padri.

Hawakuwa na jinsi, kwa kuwa hiyo ilikuwa ni siku ya tatu bila padri kuonekana, wakazunguka upande wa nyuma na kuingia. Walichokutana nacho kiliwashtua kupita kawaida, waliiona maiti ya padri ikiwa sakafuni, ilikuwa imechomwa visu kadhaa shingoni na ubavuni huku ikianza kuharibika na kuutoa harufu mbaya na kali.

Picha iliyoonekana mahali hapo iliwasisimua sana kwani mbali na kuuawa, ilionekana kabisa kwamba mwili wake uliburuzwa na hivyo kuacha alama za michirizi ya damu kitu kilichowafanya kusisimka zaidi.

“Mungu wangu! Padri!” alisema jamaa mmoja huku akionekana kushtuka.

“Jamani! Nini kimetokea?” aliuliza msichana mmoja, naye mwenyewe kama alivyokuwa mwanaume yule, alichanganyikiwa.

Walichokifanya ni kupiga simu katika kituo cha polisi hapo New York katika Mtaa wa Brooklyn ambapo baada ya dakika kadhaa polisi wakafika na kwenda ndani ya chumba kile.

Harufu iliyokuwa ikitoka humo ndani, iliwashtua, ilikuwaje mtu afe ndani ya chumba halafu ichukue siku nyingi kiasi hicho mpaka kugundua, wakahisi kwamba kulikuwa na tatizo.

“Nani amefanya mauaji haya?” aliuliza polisi mmoja.

“Hatujui! Tulikuwa tukimtafuta sana padri lakini hatukumpata mpaka leo hii tumeuona huu mwili wake,” alisema mwanaume mmoja.

Mwili ukapigwa picha, polisi walihakikisha wanafanya taratibu zote zilizotakiwa kufanywa na wao kisha kuuchukua mwili kwa lengo la kuondoka nao. Wakati wakiwa wameutoa mahali pale, wakakiona kipande cha karatasi pembeni yake, wakakichukua na kuanza kukisoma, kilikuwa kidogo kilichoandikwa maneno machache yaliyosomeka ‘It is done’ kwa maana ya kazi kukamilika.

Polisi walivyokiona kipande hicho cha karatasi walishtuka, hawakuamini kama kweli muuaji aliyekuwa amefanya mauaji katika nchi mbili, Misri na Ufaransa ndiye ambaye alifanya mauaji ndani ya kanisa hilo.

Wakapeana taarifa kwa njia ya simu kwamba kulikuwa na mauaji mengine yaliyokuwa yamefanyika na muuaji alikuwa yuleyule aliyeua kipindi cha nyuma kitu kilichowafanya watu wengi wawe na hofu juu ya muuaji huyo.

“Huyu ni nani?” aliuliza polisi mmoja, kwa jinsi muuaji huyo alivyoonekana kuwa hatari katika kufanya mauaji, wengi wakahisi kwamba alikuwa mwanaume aliyepitia mafunzo makubwa ya kuua na kuficha siri ya mauaji yake.

Baada ya kifo cha Padri Mathew Luke kutangazwa, watu hawakuamini kile walichokisikia. Mauaji yake yalifanana na mabilionea ambao waliuawa kipindi cha nyuma hivyo kuifanya dunia ishangae na kutaka kujua sababu ya muuaji kufanya mauaji hayo.

Kila kona gumzo lilikuwa juu ya muuaji huyo, watu hawakukubali, walitaka kupata ukweli kwamba kwa nini muuaji alifanya mauaji kwa mabilionea hao na mwisho wa siku kumuua padri ambaye kila mmoja alijua kwamba alikuwa mtu mwema, aliyewahubiria watu kuhusu maisha ya Yesu Kristo na kuwataka wote wafuate njia kuu.

FBI walichanganyikiwa, kila wakati waliita vikao, wakawasiliana na CIA na kuwaomba kufanya uchunguzi nchini Misri na Ufaransa ili kujua ni kitu gani kilitokea.

Katika sehemu hizo ambapo mauaji yalitokea, kulikuwa na majina ya wanawake wawili tofauti, nchini Misri kulikuwa na mwanaume aliyeitwa Maria Ogabugu ambaye alionekana kuwa na asili kutoka nchini Nigeria na kule Ufaransa mwanamke aliyefanya mauaji alikuwa mwanamke wa Kiislamu kwani bilionea huyo alipoingia ndani, aliongozana naye huku akiwa amevalia nikabu.

“Huyu muuaji atakuwa mwanamke! Huo ni uthibitisho wa kwanza tulioupata. Ni lazima tumtafute na tujue ni kwa namna gani tunaweza kumpata. Kitu cha kwanza kabisa ni kwenda kuzungumza na familia zao, tuwajue wanawake ambao walikuwa karibu nao, tukifanya hivyo, tutafanikiwa,” alisema ofisa mmoja wa FBI, huyo aliitwa Mark Thomson, mwanaume mwenye mwili uliojengeka ambaye kwake, kufanya upelelezi ndani ya nchi yake kilikuwa kitu kidogo na kila alipopewa kazi, ndani ya mwezi aliikamilisha.

“Basi tukaonane na familia zao!”
“Haina shida.”

Wakatumwa maofisa wawili wa kuonana na familia ya Padri Mathew huku wengine kutumwa kuonana na familia za mabilionea waliokuwa wameuawa nchini Misri na Ufaransa. Hilo halikuwa kazi kubwa, walijua kwamba kama wangezungumza na familia zao, wangepata mwanya wa kuanza kazi yao kwani mpaka kipindi hicho, hawakujua ni wapi walitakiwa kuanza, ila kwa kuwa walihisi muuaji alikuwa mwanamke, kwao, kazi ile ikaonekana kuwa ndogo kidogo.

****

Dar es Salaam, Tanzania

“Theresa! Huu ni mwaka wetu wa pili katika ndoa yetu, ungependa tufanye nini?” aliuliza mwanaume mmoja aliyeitwa kwa jina la Godfrey Kidatu, alikuwa kijana wa miaka thelathini na mbili, alikuwa na mwili uliojazia kidogo, kwenye kidevu chake kilikuwa na ndevu chache kidogo.

Alikuwa amekaa katika meza ya chakula pamoja na familia yake katika Ufukwe wa Miladiva. ­­­­­­Mkewe, Theresa alikuwa pembeni huku wakiwa na mtoto wao aliyekuwa na miaka miwili. Kwa jinsi walivyokaa kimahaba, kila mtu aliyekuwa katika ufukwe huo uliokuwa jijini Dar es Salaam alikuwa akiwaangalia kwani walionekana kupendeza na kumvutia kila mtu.

“Tuna mengi ya kufanya ila kwanza haka katoto kaanze shule ya chekechea,” alijibu Theresa huku akimwangalia mume wake.

Godfrey Kidatu alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na maisha mazuri jijini Dar es Salaam, alikuwa mmoja wa wafanyabiashara wakubwa waliokuwa na mafanikio makubwa katika umri mdogo.

Alikuwa kijana mcheshi, mwenye biashara nyingi zilizomuingizia kiasi kikubwa cha pesa kila siku. Maishani mwake, alikuwa na kila kitu, alikuwa na uwezo wa kufanya kitu chochote kile kwa sababu tu alikuwa na fedha.

Alijenga jumba kubwa Masaki, alikuwa na boti mbili zilizokuwa zikifanya safari kwenda katika Visiwa vya Zanzibar, alikuwa na mabasi makubwa yaliyokuwa yakienda mikoani, kwa kifupi, maishani mwake hakuwa na shida na kila kitu alichokifanya kilimaanisha pesa.

Aliamua kutoka na mkewe kwenda katika ufukwe huo, hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza ndani ya mwaka mmoja. Alitamani sana kuwa na familia yake karibu lakini kutokana na majukumu aliyokuwa nayo, hakuwa akipata nafasi hiyo hata kidogo.

Siku hiyo alipata nafasi na kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kutoka na familia yake hiyo ambayo ilikuwa kila kitu. Walikaa na kuzungumza huku kila mmoja akionekana kuwa na furaha tele, walitaniana na kufanya mambo mengi ya kimahaba, wakapanga mipango yao mengi, kwa kifupi, kila mmoja alitamani kumfurahisha mwenzake siku hiyo.

“Ila kuna kitu nataka kukwambia,” alisema Godfrey huku akimwangalia mke wake.

“Kitu gani?”
“Unalikumbuka lile dili la kusafirisha mchanga wa dhahabu nililokuwa nalihangaikia?” aliuliza Godfrey.

“Ndiyo!”
“Dili limetiki!”
“Unasema kweli?”
“Yeah! Nilipigiwa simu na kuambiwa kwamba nipo huru kufanya biashara hiyo na ile ya kuleta mafuta kupitia kampuni yetu mpya ya GoThe Oil Company. Nitakuwa nikileta mafuta na kuyasambaza sehemu mbalimbali hapa,” alisema Godfrey.

“Kweli?”
“Hahah! Mimi mzee wa madili! Ni jambo la kumshukuru sana Mungu,” alisema Godfrey, Theresa akasimama na kumkumbatia.

Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake kila siku, alikuwa mtu wa biashara, alihangaika huku na kule kutafuta pesa, hakutaka kukaa nyumbani, alikuwa akipambana huku na kule kutafuta pesa kwani aliamini kwamba hasingeweza kufanikiwa kama angekaa tu nyumbani hivyo kupambana kwa kila hali kutafuta pesa.

Hakuchoka, hakulala, kila siku alikuwa akitoka huku na kule. Hakutaka kuona akishindwa, alipambana kila siku na kumfanya kuwa miongoni mwa mabilionea wakubwa nchini Tanzania.

Walizungumza mambo mengi, wakati akiwa kwenye mazungumzo hayo, ghafla akasikia simu yake ikianza kuita, alipoangalia jina, ilikuwa simu kutoka kwa mfanyabiashara mwenzake, Majeed Khan, Muhindi aliyekuwa akipanga naye mipango mikubwa ya kibiashara.

Hakukuwa na usikivu mahali hapo, akamuonyeshea mkewe kioo cha simu na kumwambia kwamba alitakiwa kutoka hapo na kwenda kuzungumza naye kitu ambacho hakikuwa na tatizo lolote lile.

Akatoka sehemu hiyo iliyokuwa ikisikika muziki kwa sauti ya juu na kwenda upande mwingine kabisa na kuanza kuzungumza naye. Walizungumza kwa dakika kadhaa huku wakicheka kwani Khan ndiye aliyekuwa akifanya naye michongo yote ya biashara.

“Samahani kaka!” alisema mwanaume mmoja kwa sauti nyembamba huku akitaka kupita mbele ya Godfrey kwani pale alipokuwa amesimama, aliziba njia kutoka na umbo lake kuwa kubwa na sehemu hiyo kuwa ndogo.

“Hakuna shida!”

Akarudi kwa nyuma kidogo na kumpisha mwanaume huyo ambaye naye alipita upandeupande huku akimpa mgongo Godfrey, kilichomshangaza, bila aibu yoyote ile mwanaume huyo akamgusa eneo la zipu na kumtekenya kidogo.

“Wewe vipi?” aliuliza Godfrey lakini mwanaume huyo hakuzungumza kitu zaidi ya kutoa tabasamu na kuelekea alipokuwa akielekea.

Godfrey alibaki pale alipokuwa, alisimama huku akimwangalia mwanaume yule. Kwa kumwangalia, alionekana kama mtu aliyekamilika lakini alipomwangalia vizuri, akagundua kwamba hakuwa sawa, alikuwa mwanaume aliyekuwa na tabia za kikekike.

Kichwa chake kilichanganyikiwa. Katika maisha yake yote, Godfrey hakuwa mtu wa wanawake, hata kumuoa Theresa ni kwa sababu tu alitakiwa kufanya hivyo.

Katika utajiri mkubwa aliokuwa nao, hakuwa akitembea na wanawake, wengi walijigonga kwake na kumwambia kuhusu hisia zao lakini hakuwa akishughulika nao hata kidogo.

Ugonjwa wake mkubwa ulikuwa ni wa kutembea na wanaume wenzake, alipenda mambo ya mapenzi ya jinsia moja, kila alipokuwa akimuona mwanaume aliyekuwa kwenye hali ya uanawake, alichanganyikiwa na wakati mwingine alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile kumpata.

“Haiwezekani! Huyu simuachi,” alijisemea huku akimwangalia mwanaume yule aliyevalia kipensi kifupi, nywele zake alizipaka kalikiti na macho yake alikuwa akiyarembua mithili ya mwanamke aliyekula kungu.

“Call me my sweetie,” (nipigie mpenzi) alisema mwanaume yule kwa sauti nyembemba zaidi huku akiweka kidole cha gumba karibu na sikio na kidogo karibu na mdomo wake kumaanisha kwamba alitaka kupigiwa simu.

“I ain’t got your number,” (sina namba yako!) alisema Godfrey huku akimwangalia mwanaume huyo aliyeingia ndani ya gari.

“I will call you,” (nitakupigia) alisema mwanaume huyo, akawasha gari na kuondoka mahali hapo.

Godfrey akarudi kwenye kiti chake huku akionekana kuchanganyikiwa mno, kichwa chake kilikuwa kikimuwaza mwanaume tata aliyekutana naye.

Alikuwa kwenye mawazo tele, huo ndiyo ulikuwa ugonjwa wake, hakuwa na hamu na wanawake hata mara moja. Kitendo cha kukutana na mwanaume huyo mwenye sura nzuri kilimpagawisha kupita kawaida.

Theresa alimwangalia mume wake, aligundua kwamba kulikuwa na tatizo, hakuwa sawa, alionekana kuwa kwenye lindi la mawazo kupita kawaida. Hakutaka kumuacha hivyo, alimuuliza tatizo lilikuwa nini lakini hakujibu zaidi ya kumwambia kwamba alikuwa kawaida.

“Haiwezekani! Niambie kuna nini mpenzi,” alimwambia mumewe.

“Hakuna kitu!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Dili bado lipo mezani au wamelifuta?”
“Yote yapo mezani mke wangu!”

Hawakukaa mahali hapo, wakaondoka. Muda wote alikuwa akiangalia simu yake, alitaka kuona mwanaume huyo akimpigia na kumwambia mahali alipokuwa akipatikana kwani alijua kabisa kwamba asingelala, asingekula kwa sababu yake.

Kama ambavyo mwanaume anayependa wanawake anapokutana na msichana mzuri, akampa namba na kutaka kupigiwa, jinsi alivyokuwa akisubiri kwa presha ndivyo ambavyo alivyokuwa akisubiri kwa presha kubwa.

“Mbona hanipigii zaidi ya kunitamanisha tu! Mtoto ameumbika sana, ana miguu membamba lakini hapa kiunoni amekaa poa sana. Naomba anipigie tu! Ila namba yangu anayo kweli au aliniambia vile kama kunitega?” alijiuliza Godfrey, hakupata jibu.

Aliendelea kusubiri, aliisubiria simu ya mwanaume huyo zaidi ya alivyokuwa akisubiri dili za kuanza kufanya biashara zake. Siku ya kwanza ikakatika, ya pili, ya tatu mpaka wiki hakuwa amepigiwa simu kitu kilichomfanya kuukosa amani, hata safari zake za kwenda Marekani na Uarabuni hazikuwa na furaha tena, muda wote moyo wake ulikuwa ukimuwaza mwanaume huyo tu aliyekuwa na muonekano kama wa kike, alikuwa shoga.

****

Godfrey aliendelea kusubiri mpaka akakata tamaa. Miezi mitatu ilipita lakini hakuwa amepigiwa simu na mwanaume huyo hivyo kuona kwamba ilishindikana hivyo kuendelea na maisha yake.

Maisha yake hayakubadilika, kila siku aliwatamani wanaume wenzake, hakuwa na muda na wanawake, kwake, maisha yalionekana kuwa tofauti, wakati wanaume wenzake wakiwatamani wanawake, kwake, aliwatamani sana wanaume kuliko wanawake.

Alikwenda nchini Marekani, huko, kazi yake kubwa ilikuwa ni kulala na wanaume na kufanya nao mapenzi. Alijua kwamba ilikuwa dhambi kubwa lakini hakutaka kuacha, yalikuwa ni maisha ambayo aliyazoea, ikawa tabia yake na kumganda kama ruba.

Baada ya kupita miezi sita tena huku akiwa barani Asia ndipo akatumiwa meseji katika akaunti yake ya WhatsApp, harakaharaka akaifungua na kuisoma, alitumiwa kupitia namba ngeni na ujumbe aliotumiwa ulikuwa mfupi tu uliosomeka ‘Miladiva’.

Kitu cha kwanza kabisa kumjia kichwani mwake kilikuwa ni kukumbuka kitu kilichotokea kwenye ufukwe huo. Alikumbuka kwamba mara ya mwisho kwenda katika ufukwe huo ni miezi kadhaa iliyopita ambapo alikwenda pamoja na familia yake.

Hakujua ujumbe huo ulimaanisha nini lakini alipouliza, akatumiwa ujumbe mwingine mfupi uliosomeka ‘Nipigie’, hapo ndipo akakumbuka, picha ya mwanaume tata yule aliyemwambia ampigie ikamjia kichwani mwake, hakutaka kuchelewa, akamtumia meseji ya kulalamika kwamba ilichukua muda mrefu mpaka kumtafuta.

“Nilikuwa bize sana. Ila nimekumiss baba watoto,” aliusoma ujumbe huo, mwili ukamsisimka.

“Kweli?” aliuliza.

“Ndiyo! Naomba nikuone jamani!” aliusoma ujumbe huo ambao uliambatanishwa na sauti iliyorekodiwa, alipoifungua, ilikuwa sauti ya mwanaume huyo iliyokuwa ikilalamika kimahaba, tena mbali na hiyo, alimwambia kwamba alihitaji mpenzi wa kudumu kwani wapenzi wote aliokuwa nao waliishia kumtenda tu, hawakuwa na mapenzi ya dhati.

“Nipo kwa ajili yako! Nitakulinda mpenzi! Naomba kuonana nawe nikifika Tanzania,” alimwambia.

“Kwani upo wapi?”
“Nipo Kuwait, kuna kitu nimefuata.”
“Basi sawa baba watoto! Nakupenda!”

“Nakupenda pia. Mwaaaaah!”

“Mwaaaah!”

Wakaagana, Godfrey hakuamini kama aliwasiliana na mwanaume tata huyo, alibaki hotelini huku akiwa amechanganyikiwa kwa furaha, aliinuka na kuanza kurukaruka, alikuwa na hamu ya kupata mawasiliano na mwanaume huyo na mwisho wa siku alipigiwa na hivyo kuwa na namba yake.

Wakati akiwa anafurahia akasikia simu yake ikilia na alipoifungua akakutana na picha za kihasarahasara alizotumiwa katika akaunti yake ya WhatsApp ambazo zilimuonyesha mwanaume huyo akiwa katika mikao ya hatarihatari.

Japokuwa alikwenda Kuwait kukaa kwa wiki moja na kutakiwa kwenda nchini Uingereza lakini wiki moja akaiona kuwa kama mwaka, kila siku kazi yake ilikuwa ni kuangalia kalenda, hakukuwa na kipindi alichokiona siku kwenda taratibu kama kipindi hicho.

Baada ya wiki moja kukatika na kutakiwa kuelekea nchini Uingereza, hakutaka kwenda huko, hakukubali, mtu aliyekuwa akimkumbuka alikuwa mwanaume huyo aliyeitwa Fareed Hassan lakini alilibadilisha jina lake na kujiita Anti Farida.
Alipofika Tanzania, hata kabla ya kuelekea nyumbani kwake, akampigia simu Fareed na kumwambia kwamba alikwishafika nchini Tanzania hivyo alitaka kuonana naye.

“Sawa. Niambie nije wapi mpenzi?”
“Njoo hapa Dragon Fire, nitakuwepo chumba namba 20, ukija niambie niwaambie wakuruhusu,” alisema Godfrey.

Akaelekea katika hoteli hiyo, kwa kuwa alikuwa amekwishaweka oda, akaelekea katika chumba hicho na kuanza kumsubiri Fareed kwa hamu kubwa. Kila wakati alikuwa akimcheki kwenye simu kujua alifikia wapi, alitaka kumuona haraka sana kwani hakukuwa na mtu aliyekuwa na kiu ya kumuona kama mwanaume huyo.

“Nakuja jamaniiiiiii!” alisema Fareed.

“Basi wahi kipenzi! Si unajua nina kiu ya kukuona.”
“Wala usijali senyorita.”
Baada ya nusu saa akafika katika hoteli hiyo, akamwambia kwenye simu kwamba alikuwa mapokezi na hivyo kuwataka wamruhusu na kufanya hivyo. Kila mtu aliyekuwa akimwangalia Fareed, alimshangaa, alionekana kuwa na muonekano wa kike, na hata kama ungeambiwa kwamba mtu huyo alikuwa mwanaume ungebisha.

Alitembea kwa mikogo, alipokuwa akipandisha ngazi, alipandisha kwa mbwembwe huku akijitahidi kujitingisha kwa nyuma. Hakuacha kioo chake, wakati akipandisha ngazi, alikitoa kutoka kwenye mkoba wake, akatoa na lipstiki na kisha kuanza kujipaka, kila mtu aliyemuona, aliuona mwisho wa dunia.

“Jamani dunia imekwisha…” alisikika mteja mmoja.

“Kweli kabisa. Ukiwa na mtoto wa hivi! Wewe muue tu kama alivyofanya baba yake Gey yule mwanamuziki wa Marekani!” alisema jamaa mwingine.

“Kweli kabisa. Mwanaume kama mwanamke!”

“Sasa mbona anaelekea kule, kuna mtu anamsubiri?”
“Ndiyo! Kuna mshua ana apointimenti naye,” alisema dada wa mapokezi maneno yaliyomfanya kila mtu kushangaa na wengine kusikitika.

Alipofika katika chumba hicho, hakugonga, akaingia moja kwa moja. Godfrey alipomuona akiingia, akasimama, akamfuata na kisha kumkumbatia kwa furaha, hakuamini kama mwisho wa siku alionana na Fareed ambaye kila siku alikuwa akimwambia jinsi alivyokuwa akimmiss mpaka safari yake ya wiki moja kuonekana kama mwaka mzima.

Hayo ndiyo yalikuwa maisha ya Fareed, alikuwa mwanaume tata aliyeanzia tabia hiyo tangu akiwa mdogo. Alikuwa na muonekano mzuri, alikubalika, alijiona kuwa kama msichana mara baada ya kwenda kuishi kwa baba yake mdogo ambaye aliamua kumfanyia kitendo cha ajabu baada ya mkewe kusafiri kwenda Arusha.

Aliuanzia mchezo huyo kwa baba yake mdogo, alisikia maumivu sana kipindi cha kwanza lakini kikafika kipindi ambacho alizoea kabisa, akaharibika, kila kitu kilichokuwa kimetokea kilikuwa siri kubwa.

Hakumwambia mtu lakini alipomchoka baba yake mdogo akaondoka nyumbani na kwenda kufanya matendo hayo nje ya nyumba hiyo. Huko ndipo akakutana na wenzake na kumwambia kwamba tabia hizo zilikuwa zinaingiza fedha kama tu angemtafuta wakala wa kumtafutia Wazungu.

Akakubaliana nao na kumpata wakala ambaye kazi yake ilikuwa ni kumtafutia wanaume sehemu mbalimbali duniani. Alipata mabwana wengi kutoka Ulaya na Marekani. Huko kote alipokuwa akisafiri, alitumiwa tiketi na gharama zote ambapo wakala wake alichukua robo.

Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, alipata kiasi kikubwa cha fedha na kwenye maisha yake alikuwa akimiliki nyumba mbili za kifahari, magari, yote hayo yalitokana na biashara yake hiyo.

Alimsikia Godfrey tangu kitambo, aliambiwa mambo mengi kwamba mwanaume huyo alikuwa akihusudu mapenzi ya jinsi moja tena kwa kugawa kiasi kikubwa cha fedha kwa wanaume tata wote aliokuwa akifanya nao mapenzi.

Alichanganyikiwa, alipenda kuwa na pesa, alitaka wanaume wote waliokuwa na pesa wawe upande wake hivyo alichokifanya ni kuanza kumfuatilia.

Akafanikiwa kupata namba yake ya simu, hakutaka kumpigia kwa kuogopa maswali mengi ila alichokifanya ni kuwaambia marafiki zake kwamba popote pale ambapo wangemuona Godfrey basi wampigie simu kumtaarifu.
“Leo nimemuona hapa Miladiva,” alisema rafiki yake kwenye simu.

“Yupo?”
“Ndiyo! Ila na familia yake!”
“Nakuja! Nilivyokuwa na hamu naye. Nakuja!” alisema Fareed na kukata simu.

ITAENDELEA SIKU YA KESHO HAPA HAPA

Leave A Reply