The House of Favourite Newspapers

Mimi Mars atoa ya moyoni

0

MSANII wa kike kunako Bongo Flevani, Mimi Mars ameyatoa yake ya moyoni kwa wadau wa muziki nchini Tanzania ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa hawawaheshimu wasanii wa ndani ya nchi, badala yake wanawaheshimu na kuwashobokea wale wanaotoka nje ya Bongo.

 

Kupitia Insta Story yake, Mimi Mars ameandika; “Kwa yeyote itakayemhusu; inabidi muanze kuwapa heshima inayostahili wasanii wenu wa nyumbani zaidi hata ya wasanii mnaowaleta kutoka nchi za nje. Ifike mahali wasanii tupaze sauti…”

 

Hata hivyo, Mimi Mars hajaweka wazi zaidi ni kitu gani ambacho kimemsababisha aseme hivyo, lakini wadukuzi wamesema ujumbe umewafikia wahusika.

STORI; IJUMAA WIKIENDA, DAR

Leave A Reply