Misaada Ya Kibinaadamu Hanang, Lake Energies Yawasaidia Wahanga Mitungi 100 Ya Gesi Ya Kupikia Na Misaada Mingine
Manyara, Hanang: Baadhi ya wafanyakazi wa Lake Energies wakiongozwa na Meneja Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Matina Nkurlu, walifika wilaya ya Hanang, mkoani Manyara na kupokelewa na Mkuu wa wilaya hiyo, Bi Janeth Mayanya na kumkabidhi msaada wa mitungi ya gesi 100 na vifaa vingine mbalimbali vya matumizi ya nyumbani kwa ajili ya wahanga wa mafuriko wa wilaya hiyo mkoani manyara. Msaada huo umetolewa takribani mwezi mmoja baada ya mafuriko makubwa yaliyotokea wilayani humo.