DEREVA wa Mkurugenzi wa Tarime Mji na Afisa Maendeleo ya Jamii jana Januari 10, 2021, walifariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka. Katika gari hilo pia alikuwemo Mkurugenzi na Afisa Mipango ambao walikimbizwa hospitali na wanaendelea kupata matibabu.