The House of Favourite Newspapers

Mo Aahidi Private Jet, Simba Champions League – Video

0

 

MWENYEKITI wa wa Bodi ya wakurugenzi wa Klabu ya Simba, Mo Dewji amesema wamejipanga na wana bajeti ya kutosha kwa ajili ya mashindani ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika na kwamba watatumia usafiri wa ndege binafsi ‘private jet’ badala ya mabasi.

 

”Sisi tukifanya bajeti ya mwaka mzima hatuingizi bajeti ya Champions league, Champions League ina bajeti yake yenyewe. Hivyo tumetenga pesa ya kutosha….. Lazima tupate Ma- Private Jets hatuwezi kusafiri na barabara,” amesema Mo Dewji.

 

Simba katika hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika itaanza na klabu ya Plateau United ya Nigeria kati ya tarehe 27-29mwezi huu wa Novemba mchezo utakaopigwa katika dimba la New Jos. Mara baada ya mchezo huo Mnyama atakuwa na mechi ya marudiano kati ya tarehe 4-6 Disemba kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.

Leave A Reply