#BREAKINGNEWS: Mr Chuzi na Wasanii Wake Wakamatwa na Polisi
MKONGWE kwenye gemu la filamu Bongo, Tuesday Kihangala ‘Mr. Chuz’ na wasanii wake wa Closed Chapter wamesekwa ndani kwa saa tatu katika kituo kikuu cha Polisi cha Lushoto mkoani Tanga.
Chanzo chetu kinaeleza kuwa wasanii hao waliitwa kituoni na kuwekwa ndani bila kuhojiwa wala kuelezwa kosa na baadae kuachiwa.
Msanii wa filamu Bongo, Tuesday Kihangala ‘Mr. Chuz’ na wasanii wake wa Closed Chapter wamesekwa ndani kwa saa tatu https://t.co/11MmaIsQEG pic.twitter.com/1QfJY7ropX
— Global Publishers (@GlobalHabari) June 30, 2017
“Tulifikishwa tukawekwa ndani bila ya kuhojiwa wala kuandika maelezo yoyote, baadae nikaitwa na kuambiwa chukua wasanii wako muende. Nilipouliza tatzo nini nikajibiwa; chukua wasanii wako muende tu,” chanzo chetu kimeitonya Global Publishers usiku huu.
Wiki 2 zikizopita, Mr. Chuzi ali trend kwenye mitandao ya kijamii baada ya kukamatwa na kohojiwa na polisi wa Lushoto kwa kudaiwa kuwadhalilisha kingono wasanii wa kike alionao Kambini huko ambako anarekodi tamthilia yake mpya ya Closed Chapter ambayo inaoneshwa TBC1.
#MrChuzi, #ClosedChapter #Lushoto. #globalpublishers #Tanga
#Tamthilia