The House of Favourite Newspapers

Mugabe Kupigiwa Kura na Bunge Ya Kutokuwa Na Imani Nae

0
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe.

Chama cha rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kinatarajiwa kuanza mchakato wa kupiga kura ya kutokuwa na imani nae.

Afisa wa Zanu-PF amesema kuwa hoja ya kumnyang’anya urais itawasilishwa bungeni leo Jumanne na mchakato wa kumg’oa madarakani unaweza kuchukua siku mbili tu.

 

Mashtaka yaliyomo kwenye hoja hiyo ni pamoja na kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 “kumpa madaraka makubwa ya kikatiba mkewe Grace, na kushindwa kuheshimu katiba”.

 

Viongozi wa kijeshi , ambao wiki iliyopita waliingilia kati kuchukua mamlaka ya nchi walisema atakutana na makamu wake wa rais wa zamani aliye uhamishoni karibuni.

 

Jeshi limesema kuwa lina mpango na Mugabe kuhusu hali ya baadae.

Jumapili, licha ya shinikizo kubwa Mugabe aliwashangaza wengi kwa kukataa kujiuzulu, na badala yake katika hotuba yake kupitia televisheni alisema kuwa ataongoza mkutano mkuu wa chama Zanu-PF.

Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

Leave A Reply