UONGOZI wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Mlele umelaani vikali kitendo cha Mwl. Jiyabo Ng’wanzalima kucharazwa viboko na Afisa Elimu Kata ya Useya kwa kinachodaiwa kuwa hakufika kazini na kuongeza kuwa kitendo hicho kinaweza kushusha morali ya ufundishaji kwa walimu.