Mwasiti Amvulia Kofia Nandy
MSANII mkongwe kunako anga la muziki mtamu wa Bongo Fleva, Mwasiti Almasi ‘Kipepeo Mweusi’ amemvulia kofia msanii mwenzake, Faustina Charles ‘Nandy’ akisema ni mpambanaji kwelikweli.
Akipiga stori na OVER ZE WEEKEND,Mwasiti anasema kuwa, tangu mwanzo alikuwa akiwaambia watu kwamba Nandy lazima atafanikiwa.
“Nilisema tangu muda mrefu; Nandy ni mpiganaji hata ukifutalia kwenye mahojiano yangu hapo nyuma nilikuwa nawaambia watu lazima atakuja kufanikiwa kutokana na jinsi anavyojituma, leo utabiri wangu umetimia,” anasema Mwasiti aliyekulia kwenye Kituo cha THT ambacho pia Nandy alilelewa kimuzi.