MWENYEKITI mpya Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James amepokelewa kwa kishindo na vijana wa UVCCM wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati akitokea mkoani Dodoma.
Hafla hiyo imefanyika jana katika ukumbi wa Vijana Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Kheri alichaguliwa rasmi kuwa mwenyekiti Desemba 13 mwaka huu katika uchaguzi uliofanyika mjini Dodoma na kuibuka mshindi kwa kupata kura 319.
Akizungumza mara baada ya mapokezi hayo, Kheri alisema ni wakati wa vijana wa jumuiya hiyo kuwa ngangari katika kupambana na rushwa inayoharibu taswira ya nchi kwani rushwa haijengi bali itawafanya vijana kuwa wasindikizaji tu katika taifa.
NA DENIS MTIMA/GPL
Comments are closed.