MWILI wa Mvumbuzi wa madini ya Tanzanite, mzee Jumanne Ngoma (84) aliyefariki dunia juzi Jumatano, Januari 30, 2019, umeaswaliwa katika msikiti wa Masjid Maamur, Upanga jijini Dar es Salaam na kusafirishwa kuelekea kijijini kwao Makanya, Same mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko.
Mzee Ngoma alifariki katika Hospitali ya Taifa Hospitali Muhimbili (MNH) alipokuwa amelazwa akitibiwa.
Baada ya mwili huo kuswaliwa msikitini hapo waombolezaji walirudi tena Muhimbili kwa ajili ya safari ya kuelekea Makanya kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho kijijini hapo.
Comments are closed.