Rais Samia Aaga Mwili Wa Aliyekuwa Rais Wa Namibia Hayati Hage (Picha+Video)
Rais Samia Suluhu Hassan amehudhuria shughuli za mazishi ya Kitaifa ya aliyekuwa Rais wa Namibia Marehemu Dkt. Hage Geingob katika uwanja wa Michezo wa Uhuru Jijini Windhoek tarehe 24 Februari, 2024.
Hayati Rais Geingob alifariki dunia tarehe 04 Februari na anatarajiwa kuzikwa tarehe 25 Februari, 2024 katika Makaburi ya Mashujaa ya Heroes’ Acre Jijini Windhoek