The House of Favourite Newspapers

Namungo Kulipa Kisasi Kwa Nkana

0

NAMUNGO wamejinasibu kuwa, wamejipanga vizuri kulipa kisasi kwa kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo wa leo Jumapili wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Nkana.

 

Wawakilishi hao wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika, leo Jumapili wanatarajia kupambana na Nkana kwenye Uwanja wa Levy Mwanawasa, Zambia, ukiwa ni mchezo wa nne wa michuano hiyo hatua ya makundi ambapo timu hizo zipo Kundi D.

 

Katika mchezo uliopita baina ya timu hizo uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar, Namungo ilikubali kichapo cha bao 1-0.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Kocha Mkuu wa Namungo, Hemed Suleiman Morocco alisema: “Hii ni nafasi nyingine kwetu kupambana kwa ajili ya kutetea heshima ya taifa letu, tumewapa maandalizi ya kutosha vijana wetu na kufanya marekebisho ya mapungufu tuliyoyabaini katika michezo iliyopita.

 

“Kila mchezo kwetu ni nafasi ya kujifunza kwa kuwa hii ni mara ya kwanza kushiriki mashindano haya makubwa, hivyo tutapambana kuona tunapata matokeo mazuri, kama walitufunga kwetu basi na sisi tunaweza kupata matokeo bora kwao.”

STORI: JOEL THOMAS,Dar es Salaam

Leave A Reply