Nay wa Mitego Aitwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) – Video
Mwanamuziki Nay wa Mitego amesema kuwa amepokea wito wa kufikia ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kutokana na wimbo wake unaokwenda kwa jina ‘Amkeni’ alioutoa hivi karibuni.
Nay ameweka wazi kuwa alihitajika kufika leo Julai 27, 2023 saa nne asubuhi ila hakuweza kwani yuko safarini.
Nay ameongeza kuwa Mwanasheria wake ameshafanya mawasiliano na BASATA kuwaomba siku nyingine.