Ndugai Awaomba Radhi Wakristo Kwa Kauli Yake
SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amewaomba radhi Wakristo kwa kauli aliyotoa leo Bungeni alipokuwa akielezea alivyotembelea Israel
Katika maelezo yake alisema “Yesu alitembea na mke wake kutoka Nazareti kwenda Yerusalemu kuhesabiwa” ambapo amesema alimaanisha Yusufu alitembea na mke wake, sio Yesu kama alivyotamka
Amesema kilichotokea ni kosa la kibinadamu wakati alipokuwa akieleza kuwa anaufahamu ukristo vizuri na kuwa amewahi kuhiji maeneo matakatifu