The House of Favourite Newspapers

Ndugu Wa Mtanzania Aliyeuawa Kwa Risasi Marekani, Wamwaga Machozi-Video

0

Kijana wa Kitanzania aliyekuwa akiishi nchini Marekani na wazazi wake, Humphrey Magwira amepigwa risasi na kuuawa katika eneo la Fort Bend County, Houston katika Jimbo la Texas nchini Marekani.

 

Kwa mujibu wa taarifa kutoka mamlaka husika, Humphrey ambaye alikuwa ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Houston, alifikwa na mauti Ijumaa, Oktoba 15, mchana jirani na makutano ya Barabara za Beechnut na Addicks Clodine.

 

Chanzo cha tukio hilo, kinaelezwa kuwa ni ajali ndogo iliyokuwa imetokea kwa magari mawili, likiwemo alilokuwa akiendesha marehemu Humphrey, kugongana katika eneo hilo.

 

Ndani ya sekunde chache, dereva wa gari la pili aliyetambuliwa kwa jina la Ramon Vasquez mwenye umri wa miaka 19, aliteremka na kufyatua risasi kadhaa, zilizomjeruhi vibaya kijana huyo.

 

Baada ya tukio hilo, askari wa uokoaji walimkimbiza Humphrey hospitali kwa kutumia helikopta lakini muda mfupi baadaye, madaktari walithibitisha kwamba tayari amefariki dunia.

 

Dereva huyo, baada ya kutenda unyama huo, alikimbia eneo la tukio kwa kutumia gari lake lakini saa 24 baadaye, Jumamosi asubuhi, polisi walifanikiwa kumkamata.

Leave A Reply