Nicki Minaj Apata Mtoto
IMERIPOTIWA kuwa mwanamuziki Nicki Minaj na mpenzi wake, Kenneth Petty, wamepata mtoto wao wa kwanza baada ya Nicki kujifungua siku ya jana huko Los Angeles.
Nicki ali-share kwa mara ya kwanza kuwa ni mjamzito na anatarajia mtoto mwezi wa Julai mwaka huu. Pamoja na ku-post picha zake akiwa mjamzito kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Hata hivyo, mpaka sasa bado jinsia wala jina la mtoto huyo havijawekwa wazi.