Nmb Yawa benki Ya Kwanza Nchini Kusajili Wanachama wa Yanga
Kwa kutambua umuhimu wa sekta ya michezo nchini, leo @nmbtanzania imeingia makubaliano na timu ya @yangasc na kuwa Benki ya kwanza nchini kuwawezesha mashabiki na wanachama wa Yanga kupata kadi za uanachama kupitia matawi yote ya NMB yaliyoenea nchi nzima.
Baada ya kusaini makubaliano haya, ushirikiano wa NMB na Yanga utalenga maeneo yafuatayo:









Makubaliano haya yamesainiwa na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara NMB – Filbert Mponzi na Rais wa Klabu ya Yanga – Eng. Hersi Said na kushuhudiwa na viongozi wengine wa Benki na Klabu.
Usajili huu utaanza rasmi Julai 10, 2023 kwenye matawi yote ya NMB. Tembelea tawi la NMB lililo karibu yako kupata maelezo zaidi.
|