The House of Favourite Newspapers

Oya Mwana Usifanye Bifu na Mtu Fanya na Shetani!

0

Mambo vipi wazazi? Kama mpo biyee si ndo mpango mzima? Mi nipo striiti kitambo kinoma so nanyaka nini kinahapeni sasa hivi kozi kitu cha mwezi dume kinazingua ileile bati msikate tamaa masela, iwe ni chalenji dheni tuongeze kuhaso kozi mambo matamu yanatimba suuni. Ama nene makachala? Welikamu kwa sana jamvini tukisanue arifu.

Tudei bana ngoja niwasanue ishu moko inayowasebenza chama langu la washkaji. Mnajua wana haya mambo ya kupapatikia maishu ya malavu kila dei kuna kichwa kinaumia kinoma. Unajua haya malaifu ya kupeana mavibendi ambayo hayana maplani matokeo yake ndo hivo yanaleta machungu kutegemeana maelewano hafifu ya wahusika.

Baada ya kuwa napokea makompleini lukuki hapa kwa fasi ya jamvini kuhusu kuzinguana, nikaona nifanye kitu cha uchunguzi kujua nini hasa kinahapeni?

Nimenyaka kwamba maduu wengi, na hapa haijalishi wa tauni au kileji, wanaamini kuwa ili kumkamata chama lake kwa ajili ya ndoa ni kumlegezea mwana aharibu. Wanapoona kama selaa hasomeki dheni wanasema kama mbwai mbwai tu, bora wawategeshee kibendi laivu ili ijulikane moja.

Bati siyo kwa mashori tu, nang’atwa sikio kuwa wapo hata mameni ambao nao hufanya hivyohivyo wakijipa mahopu kuwa nao wanawatuliza maduu hasa wale wanaojifanya machinoo!

Kama nilivyotonya bifoo, inapotokea sasa mameni wameharibu na hawakuwa na maplani ndo unasikia msela karuka futi jiti kwamba mzigo siyo wake sema katika deizi tulizonazo mambo ya DNA yanaweka kitu pleini kwa mahewa so hakuna ishu za kudai wameba-mbikiwa.

Inapotokea ishu kama hiyo na shori akawa hana mauwezo ya kupima DNA ndo unasikia bana msela kaniharibia laifu na kuonekana shori siyo kwenye jamii.

Mazee nimeshakutana na mashori kibwena waliofanyiwa ndivyo sivyo na mameni so usipime kozi wanawachukia mameni kupita maelezo kwa kigezo kwamba wote ticha wao ni mmoko. Unakuta wakiwakea mabifu yasiyo na mpango badala ya kuweka bifu na kitu cha shetani kilichosababisha hayo yote yakahapeni.

Bati wana wakati mameni na masela wakiharibu kwani wanakuwa hawajui matokeo? Mara kibwena nimeshawasanua wana kwamba wakati wa kukubaliana kuingia kwenye maishu kama hayo ni beta wasiendeshwe na mihemko nini na nini badala yake waseto na kufanya makalukulesheni kabisa.

Mastori fekelo kama haya masela yanazingua kinoma na samtaimu wapo makiksi wanaomua bora wajitoe kitu cha pumzi wafutike kabisa kwenye feisi ya dunia au wanapojifungua ndo unasikia zile stori za kichanga kilichotupwa bila hatia aisee. Wana asikudanganye kichwa ile damu haipotei bure ipo dei itawazingua tu.

Ebana mmenisoma washkaji zangu? Kama vipi teki keya

Leave A Reply