The House of Favourite Newspapers

Oya mzazi… kikapu cha sadaka hakitoi chenji!

0

Inakuwaje wanyama wangu? Ebana ndo kama ivo kitaani kumenuka mbaya aisee chaliiangu! Pipo hawasomeki kabisa si unajua mambo ya kutumbuliwa majipu? Mazee washua kibao matumbo yapo hoti kinoma kozi famile nazo hazina uhakika wa lile laifu la kitonga walilozoea aisee arifu.

Kama vepe tumwache prezidaa Magu afanye yake kitaa kinamsapoti kozi wana wamechoka kupigwa bakora na makidi wa wanene. Mbona pipo watanyooka tu dhisi taimu?
Wakati tunamingo na laifu bila kusanda, masti tupige na mastori ya saidi bee ili mchanyato ukamilike. Wanangu si mnanyaka kuwa mambo hayaendi kwa kuangalia tu upande mmoko?
Masela tukubaliane kwamba laifu la yestadei haliwezi kufafana na tudei na hatuwezi kufanikiwa kama tukiendelea kupiga mbishe zetu kwa staili ileile kwa miaka kibwena.
Oyoo…ngoja makachala na maduu tuendelee kusebenza na mastori yetu ya kitaani pamoko na bonge la bojo yaani ni fulu mafuriko kitaa cha mabondeni.
Mazee lasti wikiendi mtu mzima niko kwenye pati f’lani hivi amezing kwa kitaa cha kishua. Unaambiwa kwenye mzigo huo hakukuwa na mtoto wa mbwa na kama kichwa kingeleta za kuleta basi kingepigwa auti fasta ndani ya dakika ziro.
Basi bana, wakati tunapiga mambo yetu, mdudu kwa pembeni na gudi miyuziki kwa mbali, si ndo shori mmoko mkare akaanza kuingia rodi baada ya mambo f’lani kukolea?
Unaambiwa mbebiz mkare akawa analeta mboyoyo mingi. Alianza kwa kunong’oneza bati kadiri taimu ilivyomuvu ndivyo alivyokuwa akipandisha kitu cha sauti chaliiangu.
Kumbe bana yule msistaduu ni mai waifu wa mtu, dheni akawa anamwaga ubuyu kuwa eti ikitokea mai hazibendi wake akavuta, ataangusha bonge la pati na kama vepe atapigwa kitu cha mereji tumoro yake! Unashangaa? Ndo kama ivo mkaksi anaamplifai kuwa amemchoka faza wa makidi wake na pembeni ameshakamatia chini msela mwingine.
Unaambiwa pipo walipigwa na masapraizi kinomanoma huku shori akiweka pleini kwamba anawishi jamaa akate ringi hata dei hiyohiyo ili ajue moko!
Akaenda fowadi zaidi kwamba eti kama ishu hiyo ikihapeni atakuwa fulu hepi kozi hana mafuraha kabisa bai dhisi taimu.
Sasa mtu mzima nikawa najiuliza, itakuwa ni misteki gani kachala aliifanya hadi shori atoe stetimenti kama ile? Wanangu tutafakari dheni tuchukue hatua na tunapokuwa kwenye kadamnasi ni vyema tukacheki na ishu za kushea na wana. Siyo sekreti yule manzi aliacha kila kichwa kikiwa kinawaza lake.
Mmenisoma chama langu? Kama shori anafikia steji kama hiyo, basi wana tusifogeti kuwa kikapu cha sadaka hakitoi chenji so ni beta kuteki keya na kuacha kufosi mambo yasiyowezekana. Rimemba maji yakishamwagika hayazoleki wanangu wenyewe!

Leave A Reply