Pango la Popo Kisarawe Lamuacha Mdomo Wazi Balozi – Video
BALOZI wa Utalii nchini, Nangasu Warema, amewaomba wadau mbalimbali wa utalii kutembelea na kujionea utalii unaopatikana ndani ya Tanzania kwani kuna vivutio vingi ambavyo wangependa kuviona.
Hayo ameyaeleza jana wakati alipotembelea Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani inayoongozwa na Jokate Mwegelo.
Nangasu aliambatana na baadhi ya wadau wa utalii akiwemo msanii wa Bongo Movies, Kulwa Kikumba maarufu kwa jina la Dude’ na msanii wa Bongo Fleva, Amini Mwinyimkuu, ambapo walitembelea vivutio hivyo vinavyopatikana wilayani Kisarawe, likiwemo pango la popo.