Mwandishi Wetu | Dar es Salaam
WAKALI wasioshikika katika Muziki wa Hip Hop Bongo, Ibrahim Musa ‘R.O.M.A Mkatoliki’ pamoja na Juma Kassim ‘Nature’ wanatarajiwa kulivuta Jiji la Dar Sikukuu ya Pasaka ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem.
Juma Kassim ‘Nature’
Akizungumza na Championi Jumatano, Meneja na Mratibu wa Dar Live, Juma Mbizo alisema kuwa, mashabiki wengi wamekuwa na hamu ya kushudia wakali hao wakipanda jukwaa moja na kulisimamisha kama wafanyavyo kwenye matamasha mengine.
Ibrahim Musa ‘R.O.M.A Mkatoliki’
“Tumesikia kilio cha mashabiki na tumewafikia, R.O.M.A usiku huo atatoa shoo ya mperampera kwa kugonga nyimbo zake zote kali kuanzia Tanzania hadi K wakati Nature akiwa na TMK Wanaume Halisi watawaonesha mashabiki staili yao mpya huku wakilichekecha jukwaa kwa vibao vikali kuanzia Mgambo, Inaniuma Sana hadi Mtumba,” alisema Mbizo.
Mbizo aliongeza kuwa mbali na wakali hao, mapema kuanzia asubuhi kutakuwa na burudani na michezo mingi kwa watot o itakayoongozwa na Kundi la Makhirikhiri kutoka Tanzania.
“Pia tutakuwa na msanii gumzo kila kona, Harmorapa wakali wa Singeli, Dulla Makabila na Msaga Sumu na wengine wengi,” alisema Mbizo.
Subscribe kwenye YouTube Chanel yetu ya Global TV Online ili zote kali zinazotufikia iwe nisiasa, michezo, comedy, burudani, stori za mastaa, muziki na nyingine kali zikufikie kwa wakati.
Comments are closed.