The House of Favourite Newspapers

RAIS MAGUFULI KUZINDUA FLYOVER YA TAZARA KESHO

RAIS Dkt. John Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Daraja la Juu ‘flyover’ mpya iliyojesgwa hivi karibuni katika makutano ya Barabara za Mandela na Nyerere katika eneo la TAZARA jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo litafanyika kesho Alhamisi, kesho Septemba 27, 2018 ambapo Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda amesema Flyover hiyo itapunguza changamoto ya msongamano barabarani iliyokuwa inaleta hasara ya Tsh. Bilioni 400 kwa mwezi.

Makonda amewaalika viongozi wa upinzani kwenda kushuhudia tukio hilo na kuwa atawawekea sehemu maalumu ya kukaa akiamini wao ndio wanaongoza kuponda maendeleo hayo na kwamba Flyover hiyo ilianza kutumika kwa majaribio mnamo Septemba 15 mwaka huu.

BREAKING: JPM Amtumbua Mwingine na Kuteua Leo

Comments are closed.