Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Taifa Stars licha ya kichapo cha 3-0 dhidi ya Morocco huku akibainisha kuwa mchezo ulikuwa mzuri lakini bahati haikuwa upande wa Stars.
“Mchezo mzuri usiku wa leo vijana wetu Taifa Stars japo bahati haikuwa upande wetu. Tunaendelea kuwatakia kila la kheri na Taifa liko nyuma yenu katika mechi zenu zinazofuata,” ameandika Dkt. Samia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii.