Rais Samia alivyowasili uwanja wa Ndege wa Ankara Esenboga Uturuki kwa ajili ya Ziara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Dkt Samia Suluhu Hassan yupo nchini Uturuki kwa ajili ya Ziara Rasmi tarehe 17 hadi 21 Aprili 2024.
Ziara inafanyika kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Uturuki, Recep Tayyip Erdoğan viongozi hao watashuhudia kusainiwa kwa Hati za Makubaliano nane (8) katika sekta za Elimu, Utalii, Utunzaji Kumbukumbu na ushirikiano katika masuala ya Diaspora.