The House of Favourite Newspapers

Rama D ‘Mfalme’ wa R&B aliyeanzia kwenye soka

0

IMG_5824

Rama D

Makala: Andrew Carlos

UKITAJIWA jina la Ramadhan Shaibu kisha ukaambiwa ni mfalme wa Muziki wa R&B nchini ni wazi utakataa hakuna msanii kama huyo, na ukiambiwa kuwa mara nyingi hutumia muda wake kuwa Brisbane, Australia na familia yake bado utakataa.

Lakini ukitajiwa jina la Rama D bila kumalizia utadakia na kusema kuwa unamjua na ni bonge la msanii wa R&B Bongo kuwahi kutokea, moja kwa moja utaanza kumsifia kwa sauti yake ilivyotumika vyema kwenye wimbo wa Nikki wa Pili uitwao Good Boy na baada ya hapo utataja listi ndefu ya nyimbo zake zikiwemo Sio Waoaji, Kama Huwezi, Kikao cha Family, Kuwa na Subira, Usihofie Wachaga, Make Up na wa sasa ambao ni Kipenda Roho.   IMG_5616

Rama D

Over Ze Weekend lilipata fursa ya kufanya makala ‘exclusive’ kutoka Brisbane, Australia ambapo yupo kwa sasa na familia yake akiwa ameoa Mzungu na kufanikiwa kuwa na mtoto mmoja.

Katika makala haya anafunguka zaidi;

 

Safari ya muziki

“Muziki nilianza kama utani, nakumbuka zamani nilikuwa napenda sana kusikiliza miziki ya aina yote, nikawa naimba kwenye sherehe za kuzaliwa ‘birthday’ za marafiki zangu huku nikitumia midundo ya Nate Dogg (marehemu), Tyrese na wengine kibao.

“Baadaye nikahamia kwenye soka, lile eneo la Mlimani City kulikuwa na uwanja wa mpira ambapo nilikuwa mchezaji wa Timu ya Survey. Sasa kila siku nikirudi kutoka mpirani njia yangu kubwa ilikuwa ni lazima nikatize nyumbani kwa kina Mr. Paul (mwimbaji wa zamani wa R&B) na niki-katiza dirishani kwake nilikuwa nikimsikia akiimba ‘akapera’ kwa sauti kubwa, nikajiuliza hivi anavyoimba huyu si hata mi naweza? Basi nikajaribu kuingia studio ikawezekana lakini kuimba kwangu kukawa ni kwa kujifurahisha tu.

 535661_594201670609340_1088683190_n

Rama D akiwa na mkewe na mwanaye

Unazungumziaje Muziki wa R&B Bongo?

“Wasanii wengi wa R&B nchini kwa sasa wanafanya poa nawasikia ni kitu cha kujipongeza hasa sisi Wabongo kuuelewa muziki huu kwani mwanzoni wengi waliutenga na kubaki kuwa ni muziki wa watu wachache.

 IMG_5840

Kwa nini wana Bongo Fleva wengi hukimbilia kurekodi nje ya nchi?

“Ujue kila mfanyabiashara anakuwa na lengo lake. Mwingine anataka kufanya video nje ya nchi ili mastaa waweze kumuona. Unakuta mtayarishaji wa video wa Sauz ana mawasiliano mazuri na vituo vikubwa vya TV kwa hiyo msanii wa Bongo anakimbilia hapo kwa kuamini atajitangaza Afrika nzima.

“Ushauri wangu kwao, kwanza tusiwe na haraka za kukimbilia huko, pili tuwakubali watayarishaji wetu na tuwape bajeti ambayo watakutengenezea video unavyotaka iwe.

 

Staa gani unamkubali kimataifa?

“Nampenda sana mdada mmoja hivi wa Nigeria anaitwa Asa, yupo vizuri kuimba na mashairi.

“Pia nawapenda sana Sauti Sol na naamini kabisa ipo siku nitakuja kufanya nao kolabo kwani wao ni waimbaji wazuri na wakikutana na mwanamuziki mzuri kama mimi lazima kitu kitoke kizuri zaidi,” anamaliza Rama D.

Leave A Reply