The House of Favourite Newspapers

RAY AJITOLEA MAISHA KWA MWANAYE

Mtoto wa Ray, Jaden.

 

MWIGIZAJI wa kiume wa Bongo Movies, Vincent Kigosi ‘Ray’ amefunguka kuwa, mwanaye aliyezaa na mwigizaji Chuchu Hans aitwaye Jaden amekuwa ndiye maisha yake kwa sababu sasa kila anachokifanya ni kwa ajili yake na amembadilisha maisha kwa kiasi kikubwa.

 

Ray na mwanaye.

 

Ray aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, ameyatoa maisha yake kwa Jaden na anafanya kazi kwa nguvu kwa ajili yake ili baadaye asipate shida kwani hatapenda afanye sanaa kama yeye.

“Maisha yangu nimemtolea mwanangu na ninafanya kazi kwa nguvu zote kwa ajili yake. Sihitaji aje kuwa msanii hata siku moja, nataka asome, afanye kazi nyingine,” alisema Ray.

 

Alichokifanya Vannesa Mlimani City Leo Hakijawahi Kutokea!

Comments are closed.