Road to Succes Yajipongeza Kufanikisha Kongamano la Wazungumzaji
Mzungumzaji wa mhamasishaji wa masuala ya mafanikio ya Kimaisha, Rodrick Nabe ametoa shukrani kwa jamaa na marafiki kwa kufanikisha kongamano za wazungumzaji lililofanyika Ukumbi wa City Mall Jijini Dar, Novemba 28 mwaka huu.
Katika kongamano hilo lililohudhuriwa na wasemaji mbalimbali ndani na nje ya nchi mgeni rasmi alikuwa Mbunge wa Jimbo la Buchosa mkoani Mwanza, Mheshimwa Eric Shigongo ambaye naye alitoa somo kwa wageni waalikwa.
Kufuatia mafanikio makubwa ya kongamano hilo Mkurugenzi wa Taasisi ya Road to Succes, Rodrick Nabe waandaaji wa kongamano hilo walifanya hafla fupi ya kupongezana.