Dar es Salaam: Msanii wa filamu za Kibongo, Husna Iddi `Sajenti’ anadaiwa kunasa ujauzito wa staa wa Singeli Bongo, Dullah Makabila anayedaiwa amekuwa akitoka naye kimapenzi.
Chanzo chetu makini kiliiambia 3 Tamu kuwa, Sajenti ni mama kijacho na mhusika ni Dullah Makabila huku baadhi ya ndugu wa Sajent wakitambua ujio wa uzao huo.
3 Tamu ilimtafuta Dullah ambaye aliomba aachwe kwanza hadi pale atakapoweka wazi mwenyewe huku Sajent akifunguka: “Inawezekana ni kweli nina mimba, hata hivyo Dullah ni mwanaume aliyekamilika, sasa tatizo liko wapi?” Alihoji Sajenti.