Sanchi: Nimeshinda Ijumaa Figa Bomba Girl 2017, Mahari Yangu Zaidi ya mil. 10
JANE Rimoy Sanchoka au Sanchi , ni jina la msanii ambaye amejizolea umaarufu mkubwa duru za burudani Bongo baada ya kuonekana kufanya vizuri katika kupamba video vya wasanii wa muziki wa Kizazi Kipya, au Bongo Fleva.
Umbo lake kubwa limemfanya kuwa kivutio, ingawa mara kadhaa wadau wamekuwa wakihoji uhalali wa chanzo cha mwili wake, wakihofu kuwa huenda anatumia madawa ya kuongeza ukubwa, ambaya yanafahamika kama ‘Mchina’. Mrembo huyoalitinga ofizi za Global TV Online katika ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori jijini Dar Jumamosi na kufanya mahojiano.
Sanchi amesema kabla ya kushinda taji la Ijumaa Figa Bomba Girl 2017 mahari yake ilikuwa Sh. milioni 10 kwa sasa mwanaume atakayefunga naye ndoa ajiandae kulipa zaidi ya Sh. milioni 20.
Kuangalia mahojiano ya Sachoka ‘Sanchi’ endelea kutembelea Global TV Online kuanzia sasa ujionee A-Z ya tukio hilo.
Subscribe hapa www.youtube.com/user/uwazi1/videos
PICHA: HILARY DAUDI, GLOBAL TV ONLINE