The House of Favourite Newspapers

Sanchoka Akubali Kumpa Penzi Idris kwa Masharti

Sanchoka

Na IMELDA MTEMA| GAZETI LA IJUMAA| STAR MIX

MODO mwenye fi ga bomba, Jane Ramoy ‘Sanchi’ ameweka wazi kuwa, sasa amekubali rasmi kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na mchekeshaji ambaye pia ni Mtangazaji wa Redio Choice FM ya jijini Dar, Idris Sultan lakini kwa masharti.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Sanchi alisema:

“Ni kweli nilikutana na Idris kipindi f’lani kule Sauzi, akaonesha kunipenda na mimi nikavutiwa naye hivyo tukaanzisha uhusiano. “Niliporudi Bongo nikapata taarifa kuwa bado Idris anatoka na Wema, hapo ndipo nilipoamua kumpotezea. Alikuwa akinibembeleza kuwa, hayuko naye lakini nilibaini bado wapo pamoja, nikakaa kando.

Sanchoka

“Sasa hivi nimeamini kweli wameachana hivyo sioni shida kuwa hivyo sioni shida kuwa naye kwa kuwa ni mwanaume wa aina yangu lakini masharti ni kwamba, asiwe na michepuko na pia aoneshe kunipenda kweli, nikibaini tofauti sidhani kama nitakuwa na amani,”alisema Sanchi.

Idriss

Idris aliwahi kutangaza kuwa ndiye anayemmiliki mdada huyo huku akimsifia kuwa ni kifaa kuliko aliyekuwa mpenzi wake, Wema Sepetu.

Comments are closed.