Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam leo imeanza rasmi semina maalum kwa wanachama wa klabu hiyo ikiwa ni kutoa mafunzo ya mambo mbalimbali yanayoihusu Simba.
TAZAMA Muundo Mpya wa Klabu ya Simba na Mabadiliko ya Katiba
Semina hiyo imejikita katika kuwajengea wanachama wake uelewa mpana zaidi juu ya muundo mpya wa klabu, uliotokana na mabadiliko ya katiba yaliyofanywa na wanachama hao na kusajiliwa na Msajili wa Vilabu nchini.
Wanachama wa Simba wamejitokeza kwa wingi kwenye Ukumbi wa Mikumi uliopo kwenye eneo la Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba (PTA), Kurasini jijini Dar es Salaam ili kuhudhuria semina hiyo.
Baadhi ya viongozi wa Simba waliojitokeza kutoa mada katika semina hiyo ni pamoja na msemaji wa Klabu hiyo, Haji Manara na Mwenyekiti wa zamani wa Simba, Mzee Hassan Dalali.
NA MUSA MATEJA | GPL