WATU watano wameuwa katika shambulio la bomu lililotokea leo nje ya hoteli moja ya kitalii katikati ya Mji wa Mogadishu nchini Somalia karibu na lango la jumba la rais.
Lori lililokuwa na mabomu lililipuka nje ya hoteli hiyo iitwayo Somali Youth League (SYL). Kundi la wapiganaji wa Al-Shabaab limekiri kutekeleza shambulio hilo.
Mtu mmoja aliyeshuhudia mlipuko huo amesema kuwa ameona watu wengi wakiwa wamejeruhiwa. Amesema kuwa hoteli hiyo imeharibika vibaya na kwamba vikosi vya usalama vimewasili katika eneo hilo.
Vyombo vya habari vinasema kuwa mkutano wa usalama ulitarajiwa kufanyika katika hoteli hiyo ya SYL.
Hoteli hiyo imeshambuliwa mara kadhaa na Al-Shabaab katika miaka ya hivi karibuni.