Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) Laongeza Ngao ya Jamii Kwenye Idadi ya Mashindano Yake
Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) limeongeza Ngao ya Jamii kwenye idadi ya Mashindano yake. Sasa kutakuwa na Shindano hilo ambalo litashirikisha timu nne.
Hapo awali huu ulikuwa ni mchezo mmoja tu kama unavyofanyika nchi nyingi Duniani ukijulikana kwa majina tofauti tofauti pia.
Mashindano ya TFF
1. Ligi Kuu (NBC PL)
2. Ligi Daraja la Kwanza (Championship)
3. Ligi Daraja la Pili (First League)
4. FA CUP
5. Mabingwa wa Mikoa (RCL)
6. Ngao ya Jamii.