Simba Yalamba Dili la Mil 800, Yatambulisha Basi Lake Jipya – Video
Klabu ya Simba leo Septemba 24, 2021 imeingia mkataba wa udhamini kutoka kampuni ya Africarriers wenye thamani ya Tsh. 800 milioni.
Mdhamini atatoa mabasi matatu;
🚍 Basi moja litatumiwa na Simba Senior Team
🚐 Basi la pili litatumiwa na Simba Queens
🚌 Basi la tatu litatumiwa na timu ya vijana (Simba Youth)
Wadhamini hao watakaa kifuani kwenye timu za Vijana na mabegani kwenye timu za Wanawake.