The House of Favourite Newspapers

Simulizi Ya Santi Cazorla Hadi Huruma!

0
Kiungo wa Arsenal, Mhispa­niola, Santi Cazorla.

KARIBU mwaka mmoja na nusu yupo nje ya uwanja kutokana na majeraha. Huyu ni kiungo wa Arsenal, Mhispa­niola, Santi Cazorla, lakini pamoja na ufundi wake, ameshindwa kabisa kucheza.

 

Achana na majeraha, lakini simulizi ya mateso ambayo kiungo huyo ali­pitia katika kipindi kigumu cha kuuguza jeraha lake la kifundo cha mguu, ndiyo ambayo inawasisimua na kuwahuzunisha wengi.

 

Cazorla, juzi alizun­gumzia mateso aliyopi­tia na hakika ni simanzi kubwa.

Fundi huyu am­baye ni kipenzi cha mashabiki wengi wa Ar­senal, alichanwa mguu mara nane ndani ya mwaka mmoja, kwa maana ya kufanyiwa oparesheni ili ku­jaribu kutibu tatizo linalomsumbua.

Akifanya yake Uwanjani.

C a z o r l a ameeleza kuwa ilibaki kidogo tu akatwe mguu na kuanza k u t e m b e l e a fimbo kuto­kana na kuin­giliwa na ki­rusi ambacho k i n g e w e z a kuhat ar i sh a maisha yake. Tangu hapo, alisu bir i miujiza tu kama anaweza tena kuche­za soka.

 

Lakini kutokana na kukatwa sana mguu katika oparesheni, ngozi yake ya mgu­uni ilipungua, ndipo ikalazimika atolewe ngozi kidogo ya mkono­ni na kuwekewa mguuni.

 

Mhispania huyo hajaingiza miguu yake uwanjani tangu Oktoba, mwaka jana, na ililazimika afanyiwe upasuaji mara nyingi sana, hivyo kupoteza ngozi katika kifundo chake cha mguu wa kulia.

Picha alizozitoa kwa Gazeti la Marca la nchini Hispania lililom­fanyia maho­jiano, ambazo zinaonyesha jinsi anavyopitia kipin­di kigumu, ndizo zi­lizowashtua wengi na kuona kumbe ili­kuwa asicheze tena soka!

Picha hizo zi­naonyesha mad­hara makubwa yanayoonekana mguuni, baada ya oparesheni nane ndani ya mwaka mmoja.

Zinaonesha jinsi ngozi yake i l i y o k u w a na tatuu ka­tika mkono wa kushoto, sasa ikiwa imehamia kwenye kifundo cha mguu.

Ma d a k t a r i wamemwam­bia nyota huyo mwenye mi­aka 32 kuwa ana bahati k u w e z a k u t em­bea tena bus­tanini na mtoto wake, huku pia ikionekana kuwa miujiza, kwamba anarejea dimbani mwanzoni mwa Januari.

Cazorla aliliambia Marca: “Kama umewe­za kutembea tena na mwanao bustanini, ri­dhika, waliniambia.”

 

“(Dr Mikel Sanchez) aliona kwamba nina kirusi ambacho kimekula sehemu ya mfupa katika kifundo cha mguu. Kuna sen­timita nane ambazo hazikuwepo!

“Siruhusiwi kucheza hadi Januari, lakini nitarudi uwanjani kufikia muda huo.”

 

Cazorla anaendelea na matibabu katika mji wa kwao, Salamanca nchini Hispania lakini kocha Arsene Wenger hivi karibuni al­isema yupo tayari kumkaribisha tena kiun­go huyo fundi katika kikosi chake baada ya Krismasi.

Wenger alisema: “Dalili za kwanza ni nzuri, lakini hajacheza kwa karibu mwaka mmoja na nusu.

 

“Bado hajaanza mazoezi kamili, anahitaji mechi chache katika kikosi cha wachezaji wa akiba. Kwa hiyo, nadhani kama mambo yote yatakwenda vizuri, itakuwa ni baada ya Krismasi.”

Cazorla alijiunga na Arsenal akitokea Malaga mwaka 2012, na ameshacheza mechi 129 za Ligi Kuu England, akiwa ame­beba makombe mawili ya FA.

Leave A Reply