The House of Favourite Newspapers

Taifa Stars Piga Malawi Hao, Tuendeleze Anachokifanya Mayanga

0
Kikosi cha timu ya Taifa Stars.

UKIANGALIA kwenye viwango vya soka vinavyo­tolewa kila mwe­zi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), utaikuta Tanzania ipo nafasi ya 125. Nafasi hiyo si nzuri kwani inadhihirisha kwamba tumeshuka sana na hatuna uwezo wa kupambana na vi­gogo.

 

Nakumbuka nafasi hiyo ya 125, tuliipata mwezi Agosti ikiwa ni miezi miwili imepita tangu tushike nafasi ya 116. Ukiangalia hapo ndani ya mie­zi mitatu tumeshuka kwa na­fasi tisa.

 

Si jambo la kufurahisha kuo­na kila kukicha tunaporomoka kwenye viwango vya Fifa, ki­nachotakiwa ni kuiandaa vi­zuri timu yetu ili iweze kutoa ushindani na kushinda katika michezo mbalimbali ya kirafiki na kimashindano ili ipande juu. Tutoke huku tulipo sasa.

 

Katika kuiandaa vizuri timu, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lina jukumu la kuhak­ikisha kila kwenye Kalenda ya Fifa tucheze mechi ambazo ndizo zitatupandisha kule tu­napopataka.

Kucheza mechi nyingi inawa­jengea kujiamini w a c h e z a j i ambapo hata kama ikitokea tumefungwa, basi naamini siku zijazo baa­da ya kujiamini wa t a t u l e t e a matokeo mazu­ri. Tutakuwa tu­metatua tatizo lililopo.

 

Kusema TFF ina jukumu la kutafuta mechi za kirafiki kwa Taifa Stars s i m a a n i s h i kwamba hivi sasa hawatafuti, bali ni kuendelea kufanya hivi inavyofanya sasa.

Nafahamu leo Jumamosi, Taifa Stars itakuwa na mchezo wa kirafiki uliopo kwenye Kal­enda ya Fifa dhidi ya Malawi. Mchezo huo utapigwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

 

Mchezo huo ni muhimu kwetu kwa sababu matokeo ya ushindi yat­a t u f a n y a tuwe na na­fasi nzuri ya k u p a n d a katika vi­wango vya Fifa jambo a m b a l o tumekuwa tukilihitaji kwa muda mrefu.

M b a l i n a kupanda k w e n y e viwango h i v y o , lakini pia itatu­saidia katika maandalizi yetu ya mechi za kufuzu kwa mi­chuano ya Kombe la Mataifa Afrika (Afcon) kwa mwaka 2019.

 

Tukitumia vizuri michezo hii ya kirafiki, itatupa matokeo mazuri si leo, bali hapo baa­daye kwa sababu bado kikosi chetu kipo kwenye hatua za kujengwa na kweli kinajenge­ka.

Nikiitazama Taifa Stars ya sasa, naiona bado ipo kwenye maandalizi makubwa ambayo siku zijazo kama ikiwa na mwendelezo huu basi itatufiki­sha mbali.

 

Tangu Kocha Salum May­anga akabidhiwe kikosi hicho, amekuwa akijitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha anakuwa na vijana wengi ambao watai­saidia timu hiyo kufanya vizuri.

Mayanga amekuwa na juhudi kubwa ya kuwatafuta wachezaji wa Kitanzania wa­naocheza soka nje ya Tanzania ambao siku za nyuma hawaku­wahi kuitumikia Taifa Stars.

 

Anachokifanya Mayanga ki­natakiwa kuwa na mwendele­zo hata kama ikitokea siku am­eondolewa kwenye nafasi hiyo kwa sababu tunafahamu licha ya kuaminika, lakini hatoweza kudumu milele.

Bado naamini kuna Watan­zania wengi wapo nje ya nchi hii wanacheza soka na kama wakiitwa basi watakuwa na msaada mkubwa kwa taifa letu.

Huku tukiwa tunaipam­bania Taifa Stars, tusizisahau timu zetu nyingine za taifa, kuanzia ile ya chini ya miaka 17 maarufu kama Serengeti Boys ambayo mwaka 2019 ita­shiriki michuano ya Kombe la Mataifa Afrika kwa umri huo itakayofanyika hapa Tanzania. Pia tusiisahau U-20 na U-23 pamoja na zile za wanawake.

 

Wikiendi iliyopita tu, timu yetu ya taifa ya wanawake chini ya miaka 20, Tanzanite, ilifungwa mabao 6-0 ikiwa ny­umbani katika mchezo wa ku­fuzu kwa michuano ya Kombe la Dunia dhidi ya wenzao wa Nigeria maarufu kama Fal­conets.

Kipigo hicho kinaenda sam­bamba na kile cha mabao 3-0 ambacho walikipata ugenini na kuwafanya kuondoshwa kwa jumla ya mabao 9-0.

Tukiwekeza katika timu zetu zote za taifa, naamini tutapiga hatua kuanzia soka la wasicha­na mpaka la wavulana.

Leave A Reply