Tanzia: Baba T Afariki Dunia
ALIYEKUWA Mtangazaji wa kipindi cha Lovers Rock ya East Africa Radio Baba T, amefariki dunia jana katika Hospitali ya Rabininsia iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam.
Rafiki wa karibu na marehemu Baba T, Gota Irie amesema taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi zitatolewa kwa sasa wanasubiriwa ndugu zake kutoka nje ya nchi.
Wasifu mfupi wa mtangazaji na DJ mkongwe Baba T aliyefariki jana
Jina kamili: Emsley Smith
Kuzaliwa: Desemba 28 1936, Kingston Jamaica
Alihamia Uingereza akiwa na miaka 27 na kufanya kazi kama Mhandisi na DJ, kisha Australia na baadaye Tanzania mwaka 1988.