The House of Favourite Newspapers

Tanzia: Jaji Samwel Karua Afariki Dunia

0

Familia ya Jaji Samuel Victor Gibson Karua Kwa masikitiko makubwa inawatangazia ndugu, jamaa na marafiki, Kifo cha mpendwa wao Jaji Samuel Victor Gibson Karua kilichotokea leo tarehe 26/02/2021 saa moja na nusu asubuhi (1:30) asubuhi, katika hospitali ya Saifee.

 

Msiba utakuwepo nyumbani kwa marehemu Jaji Samuel Victor Gibson Karua Kijitonyama. Ndugu wapendwa kutokana na janga linaloendelea hivi sasa ,familia inawapenda sana ila tunaomba kwa sasa familia pekee ndio ijumuike hapa nyumbani Kijitonyama na kuwaomba ndugu, jamaa na marafiki tujumuike pamoja siku ya Jumatatu kwa ajili ya kumuaga na mazishi yatakayofanyika siku hiyo nyumbani kwake Goba Michigani pia tunasisitiza uvaaji wa barakoa na kunawa mikono na kukaa mbali mbali.

 

Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa, Jina lake lihimidiwe.

Familia ya Jaji Samuel Victor Gibson Karua.

 

==========================

Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Samwel Karua amefariki dunia leo Februari 26 katika hospitali ya Seifi iliyopo Oystebay jijini Dar es salaam.

Msiba upo nyumbani kwake Kijitonyama na mipango ya mazishi itajulikana hapo baadaye.

Mahakama ya Tanzania inatoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE.

Leave A Reply