LEO Jumamosi Juni 17 zilikuwa shamra shamra za uzinduzi wa michuano ya soka la mitaani maarufu kama Ndondo Cup 2017 ambazo zimefanyika katika Uwanja wa Kinesi uliyopo Shekilango, Ubungo jijini Dar es Salaam ambapo mashabiki kibao wamejitokeza kushuhudia uzinduzi huo.
Katika uzinduzi huo, timu za Makuburi FC yenye maskani yake mtaa wa Makuburi na Stim Tosha zilishuka dimbani kumenyana vikali ambapo mchezo huo ulikuwa wa kuvutia na wenye upinzani wa aina yake.
Mashabiki wa timu zote mbili walionekana kuzisapoti timu zao mwanzo mwisho huku mbwembwe za mitaani zikichukua nafasi uwanjani hapo. Michezo mbalimbali, utani wa kiganga na kelele za kushangili ndivyo vilitawala muda wote wa mchezo huo.
Mastaa kibao waliibuka uwanjani hapo kushuhudia game hiyo wakiwemo, wanamuziki na wachezaji wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na viongozi maarufu wa soka hapa nchini.
Miongoni mwa mastaa waliohudhuria ni pamoja na Madee, Sholo Mwamba, Beki wa Yanga, Hassan Kessy, Man Fongo na wengine.
Mpaka mwisho wa mchezo huo timu zote zilitoka suluhu ya bila kufungana hivyo kugawana pointi moja kila timu.
Mchezo ukiendelea.
Ambulance likiwa tayari kwa dharula yeyote uwanjani hapo
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS | GLOBAL PUBLISHERS