The House of Favourite Newspapers

Ukweli Wote Warda Kudaiwa Kuonekana Afrika Kusini, Mazito Yaibuka Tena – Video

0
Baba wa Warda Mohammed, Mohamed Machamla

Siku chache zilizopita, ziliripotiwa habari na mtu aliyejiita msamaria mwema, kwamba amemuona msichana mdogo, Warda Mohammed (16) nchini Afrika Kusini.

Hata hivyo, baada ya kujiridhisha, Global TV imebaini kwamba mwanaume huyo alitoa taarifa za uongo kwa nia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Warda, mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyumbu, Kibaha alipotea tangu April 19, 2023 na bado jitihada za kumtafuta hazijazaa matunda.

Kwa yeyote atakayemuona au mwenye taarifa za mahali alipo, awasiliane nao kwa namba za simu ambazo ni:

0656520998 au 0687003356.

DAU LA SHILINGI MILIONI 3 LIMETANGAZWA KWA YEYOTE ATAKAYEMUONA.

Leave A Reply